Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) – Ikwiriri, Tanzania - Kiongozi Msaidizi wa Taasisi ya Hujjatul Asr Society of Tanzania, Sheikh Eid Harun, ametembelea Kituo cha Sayyidat Fatima Zahraa (a.s) kilichopo Ngomboloni – Ikwiriri kwa lengo la kuwatambulisha walimu wapya wa Madrasa hiyo.
Katika ziara hiyo, Sheikh Eid aliwapa wanafunzi nasaha kuhusu umuhimu wa kujitahidi katika masomo yao na kusisitiza nafasi ya elimu ya dini katika kujenga jamii yenye maadili mema.
Aidha, Maulana Sayyid Arif Naqvi, Kiongozi Mkuu wa Taasisi hiyo, naye ametembelea Hawza ya Imam Ridha (a.s) na alipata fursa ya kuswali Sala ya Jamaa pamoja na waumini, jambo lililopokelewa kwa furaha kubwa na wapenzi wa Ahlul-Bayt (a.s) waliokuwepo katika eneo husika.
Your Comment